Wednesday, February 13

Kumbukumbu ya Champions League

Image result for Champions League
  •  Ole Gunnar Solskjaer ameshindwa kwa mara ya kwanza kama meneja wa Man Utd katika mechi zote 12 aliyochezwa chini ya uongozi wake, hii ikiwa pia ndio kipigo kikali walichopewa nyumbani katika mashindano yoyote ya Ulaya.
  • Paris Saint-Germain ni timu ya kwanza ya Ufaransa kushinda Manchester United katika uwanja wa Old Trafford katika shindano lolote barani Ulaya kabla ya mechi ya Jumanne usiku).
  • Kwanzia mwanzo wa msimu wa mwaka 2016-17, ni Cristiano Ronaldo pekee aliyefunga mabao mengi zaidi (mabao16) katika mechi za muondoano za Champions league kuliko Kylian Mbappe wa PSG aliyefunga (mabao 7) kufikia sasa.
  • Timu 34 zilizoshindwa mechi ya kwanza ya muondoano katika Champions League hakuna hata moja iliyofungwa bao zaidi ya moja nyumbani iliyofanikiwa kuendelea mbele katika juhudi ya kuwania taji hilo.
  • Solskjaer ni meneja wa pili wa Manchester United kufungwa mechi ya kwanza ya Champions League,baada ya Louis van Gaal (Ferguson, Moyes and Mourinho wote walishinda).
  • Angel Di Maria ameandikisha rekodi ya kuchangia ufungaji mabao katika Champions League kwa mara ya tatu, na ya kwanza tangu mwezi Septemba 2013 (wakati wa mechi ya Real Madrid dhidi ya Galatasaray).
  • Gianluigi Buffon amekuwa mchezaji wa nne kucheza Champions League akiwa na mika 41 (baada ya Marco Ballotta, Mark Schwarzer na Oleksandr Shovkovskiy); Alishiriki mashaindano hayo mra ya kwanza kabla ya wachezaji Marcus Rashford na Kylian Mbappe kuzaliwa.

No comments:

Post a Comment