Thursday, May 18

Majina ya wachezaji 5 wanaowania tuzo ya mchezaji bora ligi kuu ya Vodacom (VPL)









Wachezaji watano wameteuliwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2016/2017.

Wachezaji walioteuliwa kuwania kinyang’anyiro hicho ni 
Aishi Manula (Azam Fc)


 Haruna Niyonzima (Yanga Sc)


 Mohamed Hussein (Simba Sc)


 Shiza Kichuya (Simba SC)


 na Simon Msuva (Yanga Sc)



Majina hayo yatapigiwa kura na makocha , makocha wasaidizi na manahodha wa timu za ligi kuu ya Vodacom pamija na wahariri wa michezo kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini.

Wahusika watatumiwa fomu maalum za kupiga kura kwenye email za klabu zao na vyombo husika vya habari. Mwisho wa kupiga kura ni May 23 2017 saa 6 usiku.

Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ambayo unaratibiwa na kamati ya Ushauri ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itafanyika May 24 mwaka huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment